Wednesday, November 20, 2013

Tanzania na Kenya zatiliana sahihi mkataba wa kurahisisha biashara mipakani


Mawaziri wa jumuiya ya Afrika Mashariki wa Kenya Musa Slima na wa Tanzania Samweli Sitta wakitoka kwenye ofisi ya DC Taveta kuhudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika Taveta Kenya na kuhudhuliwa na wananchi
wa Tanzania na Kenya.
-----------------------------------------------------------
Serikali za Tanzania na Kenya zimetangaza hatua kadhaa za kuwawezesha wafanyabiashara wadogo wa mipakani mwa nchi hizo kuingia katika nchi nyingine kufanya biashara bila hati ya kusafiria na wakuu wa wilaya za mipakani wameagizwa kukaa pamoja na kuandaa utaratibu utakaotumika. 
 Makubaliano hayo yamefikiwa katika wilaya ya Taveta nchini kenya na kusainiwa na mawaziri wa jumuia ya afrika mashariki Bw Samwel Sita wa Tanzania na Musa Srima wa Kenya mbele ya wananchi wa pande zote hizo katika mkutano wa hadhara ambao viongozi hao walitoa ufafanuzi juu ya hatua hizo. 
 Waziri Sita amezitaja baadhi ya hatua hizo kuwa na fomu maalum za kuwatambulisha wafanyabiashara hao kufanya biashara zao katika masoko ya jirani yaliyo ndani ya umbali wa kilomita 20 kati ya nchi na nchi wakiwemo waendesha pikipiki. Akitoa ufafanuzi waziri Srima amesema, katika makubaliano hayo maafisa forodha wa pande zote wametakiwa kutoa elimu ya kutosha kwa wafanyabiashara wakubwa ya namna uvushaji na ulipaji wa ushuru wa bidhaa zao na kuangalia uwezekano wa kufanya kazi kwa saa 24 wa idara zzote zikiwemo za uhamiaji.

Chanzo:Picha na Habari na Dixon Busagaga 
wa Globu ya Jamii, Moshi.

0 comments:

Post a Comment